Jumatatu, 21 Desemba 2015

      Umuhimu wa Maji mwilini

 Tunaambiwa kuwa maji ni muhimu sana ndani ya miili yetu. Maji yana faida nyingi sana na wengi tunazijua, lakini tutajikumbusha baadhi. Tuanze hivi, Moja maji husaidia kupunguza calories mwilini, yaani badala ya kunywa vimiminika vingine kama soda, bia na juisi ambavyo vina calories, maji hayana calories. hivyo utakua umekunywa maji ambayo ni salama mbadala na vinywaji vingine ambavyo vina calories.Kumbuka pia maji hayana sukari, mafuta na viungo vingine vinavyotengeneza vimiminika vingine

   Pili, unywaji wa maji mengi hutupunguzia uwezekano wa kupata magonjwa kama ya moyo, hivyo inashauriwa kwa siku tunywe zaidi ya bilauri mbili za maji na kuendelea. Tatu, maji huongeza nguvu mwilini kwani unapokua na upungufu wa maji, unaanza na kusikia kiu ambayo huenda kupelekea kujisikia uchovu, misuli kuchoka, kizunguzungu na ishara nyingine za kunyongonyeza mwili.
  Nne maji ni dawa ya maumivu ya kichwa. Mara kwa mara tuumwapo kichwa pengine ni upungufu wa maji ndio uliopelekea maumivu haya, lakini tunywapo maji basi maumivu huoondoka. Kuna sababu nyingine zinazopelekea vichwa vyetu kuuma lakini, ukosefu wa maji mwilini ni sababu inayojulikana zaidi.   


 Kama hatukuwahi kuwa na mazoea ya kunywa maji kwa kiwango hicho mwanzo huw ni mgumu, lakini waweza anza mdogo mdogo kwa bilauri mbili, kesho yake tatu, inayofuata nne mpaka tufikie hizo lita mbili.
   Kuna wale wenzangu na mimi watakaosema maji hayana ladha, nakupa maarifa kidogo waweza changanya na kikorombwezo upendacho kuyapa ladha ili upate hamu yakuyanywa, maana mwisho wa siku ni lazima kunywa maji, Waweza tumbukiza kijipande cha ndimu, au chungwa au kitu kingine unachopenda ladha yake

 
   Umuhimu wa Tano wa maji mwilini ni kwamba, unywaji maji hupelekea kusafisha ngozi yako, na mara kwa mara Rafiqs wengi wamejivunia kuwa na ngozi bora baada ya unywaji wa maji wa kutosha. Haiwezi tokea mara moja ila baada ya wiki moja utaanza kuona mabadiliko ya ngozi yako na itaanza kung'ara.
   Sita, mfumo wa kuchanganya chakula ndani ya miili yetu (digestive system) unahitaji maji mengi ili kufanikisha kazi yake kifasaha, hivyo yatupasa kuhakikisha mfumo huo unafanya kazi yake vyema katika muda sahihi kwa kunywa maji ya kutosha. Pia maji husaidia kuponesha maumivu ya vichomi vya tumbo, na pia hutupa urahisi pale tuendapo haja kubwa, kwani tunakua hatuna ukosefu wa maji mwilini. Maji husaidia pia kuondosha uchafu ndani ya miili yetu na kuacha mwili ukiwa msafi.
   Saba, Kwa unywaji mwingi wakati wa mfumo wa kuchanganya chakula unaendelea, imeonekana kuwa maji husaidia kupunguza uwezekani wa kupata saratani ya colon kwa asilimia 45, asilimia 50 ya saratani ya kibofu cha mkojo na pia hupunguza uwezakano wa kupata saratani ya matiti kwa kina mama.
  Nane, Kuwa na ukosefu wa maji mwilini husababisha kukurudisha nyuma katika swala zima la mazoezi na kukufanya iwe ngumu kunyanyua vyuma vya mazoezi, pamoja naa kufanya mazoezi mengine, hivyo basi inashauriwa kunywa maji kabla, wakati na baada ya mazoezi ili uweze kuyafanya vyema na katika hali salama.
 
kwa maelezo zaidi msomaji wetu wa blog hii ya lupimo sanitarium clinictufikie katika vituo vyetu vilivyopo mikoa mbalimbali hapa nchini

VITUO VYETU TUNAVYOPATIKANA LUPIMO SANITARIUM CLINIC NI KAMA IFUATAYO. IRINGA TUPO KIHESA NJIA PANDA YA MTWIVILA, MBEYA TUPO SOWETO KARIBU NA UWANJA WA SHULE YA MSINGI MWENGE, DAR ES SALAAM TUPO SINZA MORI AU SINZA MAPAMBANO NYUMA YA UKUMBI WA LULU, DODOMA TUPO AREA C KARIBU NA MSIKITI WA AREA C, SINGIDA TUPO MANYONI NJIA PANDA YA KUELEKEA CHIKOLA NA HEKA, GEITA TUPO MITI MIREFU KARIBU NA BICK HOTEL, MWANZA TUPO NYEGEZI KITUO CHA KIJIWENI AU KALFONIA,


kwa maelezo zaidi,maoni au ushauri wasiliana nasi kwa simu namba 0769368546,0719097574 na 0742120577 pia www.facebook.com/lupimoclinic,www.twitter.com/lupimoclinic na www.hulkshare.com/lupimoclinic.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni