Ijumaa, 11 Machi 2016

PENDELEA KULA MATUNDA NA MBOGAMBOGA UPATE FAIDA ZAKE

Kwa kawaida, tunatakiwa kula matunda na mboga za majani kila siku, kiasi kisichopungua milo mitano. Lakini kwa bahati mbaya sana, siyo watu wote wenye fursa ya kupata na kula matunda kila siku. Hata wale wenye fursa hiyo, hawali inavyotakiwa.
Kitendo cha kutokula matunda hukosesha miili yetu virutubisho muhimu vya kujenga na kuimarisha kinga ya mwili, matokeo yake miili yetu inakuwa haina kinga ya kutosha. Mwili unapokuwa na kinga dhaifu, ni rahisi kushambuliwa na maradhi hatari, ikiwemo saratani, ambayo kinga yake kubwa iko kwenye ulaji wa matunda na mboga za majani.

Utashangaa kuona mtu anamaliza mwezi mzima hajala hata tunda moja. Msimu wa machungwa, kwa mfano, unaingia mpaka unaisha hajala hata chungwa moja. Ukija msimu wa maembe nao ni hivyo hivyo. Kuna mazoea ya kuona matunda siyo sehemu ya vyakula muhimu. Tabia hii ndiyo chanzo cha magonjwa mengi yanayotukabili hivi sasa.

Kwa upande mwingine, kuna makosa hufanyika wakati wa kula matunda. Kitaalamu inashauriwa kula matunda tumbo likiwa tupu, yaani kabla hujala kitu chochote tanguliza matunda kwanza na baada ya nusu saa au saa moja, ndiyo unashauriwa ule mlo wako kamili.
 
 kwa maelezo zaidi,maoni au ushauri wasiliana nasi kwa simu namba 0769368546,0719097574 na 0742120577 pia www.facebook.com/lupimoclinic,www.twitter.com/lupimoclinic na www.hulkshare.com/lupimoclinictanzania.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni