Thursday, February 11, 2016
Watu 21 Watiwa Mbaroni kwa Mauaji ya Kondoo Na Mbuzi Mvomero
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Lupimo sanitarium clinic ni
kituo cha tiba asili wanatibu magonjwa kama
kuota kinyama sehemu ya haja kubwa na magonjwa mengine mengi, kutana tabibu
bingwa ambae ni mkurugenzi wa lupimo sanitarium clinic John lupimo mpigie simu
sasa hivi umweleze tatizo lako kupitia 0742120577,0769368546 au 0672666601.
WENYEVITI wa Serikali za vijiji vya Mkindo, Patrick Longomeza (52) na mwenzake wa Dihombo, Christian Thomas (50) pamoja na wananchi wengine 19 wanashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kujeruhi mifugo mali ya mwanamke mfugaji wa Kimasai, Katepoi Nuru (36) wa Kijiji cha Kambala wilayani Mvomero Mkoa wa Morogoro.
Mbali
na wenyeviti wa vijiji hivyo, pia Polisi wamemtia mbaroni kinara wa
uhamasishaji vijana wa kimasai kuwapiga na kuwajeruhi wakulima wanaolima
katika Bonde la Mgongola, Kashu Moreto (68) kwa tuhuma za kulisha mazao
na kumjeruhi mguu wa kulia, mkulima Ramadhan Juma (19), mkazi wa
Dihombo.
Kamanda
wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Leonard Paulo alisema hayo jana wakati
akizungumza na waandishi wa habari kuhusu tukio la awali lililotokea
Februari 7, mwaka huu mchana katika Kijiji cha Kambala.
Alisema
kabla ya kukatwa kwa mifugo ya mwanamke huyo, kundi la ng’ombe zaidi ya
50 likiwa na wachungaji zaidi ya watatu wa Kimasai walilisha shamba la
mpunga ekari moja la mkulima Rajab Issa (31) aliyewazuia na ghafla
walijitokeza vijana wanaosadikiwa kuwa ni Morani wa kimasai na
kuwachukua ng’ombe hao kwa nguvu.
Aliwataja
wengine waliotiwa mbaroni mbali na wenyeviti hao ni Issa Ally (66),
Hussein Said (25), Juhudi Amimu (25), Emily Pascal (40) na Mkude
Milikioni (25) ambao wote ni wakazi wa Kijiji cha Mkindo.
Wengine
waliokamatwa ni Ally Bakari (25), Gerald Mbegu (22), Miraji Noras (22),
Mengi Mbegu (32), Kudura Abdi (35), na wanawake wawili Angelina Sadiki
(20), Hadija Msanga (30), wote wakazi wa Kijiji cha Mkindo.
Pia
wamo Mustafa Malugo (35), Charles Moris (40), Amset Alfred (42), Hassan
Mohamed (46) pamoja na Hapifan Paulo ambao wote hao ni kutoka katika
Kijiji cha Dihombo wilayani Mvomero.
Kamanda
Paulo alisema baada ya vijana hao wa kimasai kuingia kulisha katika
shamba la Issa, alijaribu kuwazuia, lakini ghalfa walijitokeza vijana
wanaosadikiwa kuwa ni morani wa kimasai na kuwachukua ng’ombe hao kwa
nguvu, na mkulima huyo alitoa taarifa katika Kituo cha Polisi Mvomero.
Lakini
alisema Februari 8, mwaka huu mchana wakati tukio hilo
likishughulikiwa, kikundi cha watu kilivamia nyumbani kwa Nuru Kipande
(76) na kumkuta kumkuta Ketepoi Nuru (36) akiwa nyumbani huku mifugo
aina ya mbuzi, kondoo na ndama wakiwa malishoni.
Kwa
mujibu wa Kamanda, kundi hilo lilinyang’anya mifugo hiyo na kisha
kumnyang’anya mwanamke huyo simu yake ya mkononi ili asiombe msaada na
kisha kuipeleka mifugo hiyo porini na kuanza kuikatakata kwa vitu vyenye
ncha kali .
Kamanda
alisema watuhumiwa waliokamatwa wanaendelea kuhojiwa na wengine
kutafutwa na wote waliohusika katika tukio hilo watafikishwa mahakamani,
na kutoa onyo kwa watu wote kuacha kujichukulia sheria mkononi.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
VITUO VYETU TUNAVYOPATIKANA LUPIMO SANITARIUM CLINIC NI KAMA
IFUATAYO. IRINGA TUPO KIHESA NJIA PANDA YA MTWIVILA, MBEYA TUPO SOWETO KARIBU
NA UWANJA WA SHULE YA MSINGI MWENGE, DAR ES SALAAM TUPO SINZA MORI AU SINZA
MAPAMBANO NYUMA YA UKUMBI WA LULU, DODOMA TUPO AREA C KARIBU NA MSIKITI WA AREA
C, SINGIDA TUPO MANYONI NJIA PANDA YA KUELEKEA CHIKOLA NA HEKA, GEITA TUPO MITI
MIREFU KARIBU NA BICK HOTEL, MWANZA TUPO NYEGEZI KITUO CHA KIJIWENI AU
KALFONIA,
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni