Alhamisi, 24 Machi 2016

ZIJUE FAIDA KUMI ZA KUNYWA MAJI YA MADAFU.




Maziwa   ya  nazi, mafuta  ya  nazi  pamoja  na  maji  ya  madafu  ni  bidhaa  ama  malighafi  zinazo  tokana  na  mti  wa  mnazi. 
 




 Katika  makala  ya  leo  tutazungumza  kuhusu   maji  ya  madafu, ambapo  tutapata  kuzifahamu  faida  kumi  zitokanazo  na  kunywa  maji  ya  madafu.

Maji  ya  madafu  ni  maarufu  sana  miongoni  mwa  wenyeji  wa  mikoa  inayo  patikana  katika  ukanda  wa  pwani  ya  Tanzania.

Pamoja  na  kutumika  kama  kinywaji  kwa  ajili  ya  kuondoa  kiu, maji  ya  madafu  yana  faida  lukuki  kwa  afya  ya  mwanadamu.

Siku  ya  leo  tutapata  kuzitazama  faida  kumi  za  maji  ya  madafu.

1.   Yanazuia  Upungufu  wa  Maji  Mwilini.

2. Yanaimarisha  ubongo  na  misuli

3. Maji  ya  madafu  yanasaidia  kuzuia  muonekano  wa  kizee  
 (anti-aging ): Matumizi  ya  mara  kwa  mara  ya  maji  ya  madafu  yatakufanya  uonekane    kijana  hata  kama  umri  wako  umeenda.  Kuwa  na  uwezo  wa  kuzuia  muonekano  wa  uzee  ni  miongoni  mwa  sababu  zinazo  yafanya  maji  ya  madafu  yawe  maarufu  sana  miongoni  mwa  wasanii  wanao   igiza  filamu   huko  Hollywood  nchini  Marekani.
.
4. Maji  ya  madafu  yanasaidia kuimarisha  mfumo  wa  usagaji  chakula  tumboni.

5.Maji  ya  madafu  yanasaidia  kuimarisha  mfumo wa  kinga  ya  mwili. 

6. Maji  ya  madafu  yanasaidia  kukukinga  dhidi  ya  magonjwa  ya  moyo  pamoja na  presha.

7.  Maji  ya  madafu  yana  utajiri  mkubwa  sana  wa  vitamin  mbalimbali, amino  acids,vimen’genyo, viondoa  sumu  pamoja  na  virutubisho  mbalimbali.

8. Maji  ya  madafu  yana  kiasi  kidogo  cha  kalori


9.  Maji  ya  madafu  yanasaidia  kuunyambua  mwili.
10. Maji  ya  madafu   yana  imarisha  mzunguko  wa  damu  mwili.

UNANGOJA  NINI? ANZA  KUTUMIA  MAJI  YA  MADAFU  LEO  UPATE  FAIDA  KIBAO  ZA  KIAFYA.
 kwa maelezo zaidi,maoni au ushauri wasiliana nasi kwa simu namba 0769368546,0719097574 na 0742120577 pia www.facebook.com/lupimoclinic,www.twitter.com/lupimoclinic na www.hulkshare.com/lupimoclinictanzania,www.lupimoclinic.blogspot.com youtube.com/lupimoclinic.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni