Jumatatu, 22 Juni 2015

 
Tunaendelea kutoa elimu ya masomo mbali mbali ili wewe ambaye unasumbuliwa na maradhi tofauti tofauti uweze kupata huduma katika hatua za awali kabla ya kutufikia.
Leo hii tutazungumzia kuhusu maradhi ya kutazama maradhi yanayoathiri watu wengi zaidi nayo si mengine bali ni pumu ya ngozi au kwa kitaalamu huitwa Eczema.
Pumu ya ngozi (Eczema)
Pumu ya ngozi au kwa kitaalamu Eczema (atopic dermatitis au atopic eczema) ni maradhi ya ngozi ambayo yamefanyiwa utafiti muda mrefu sana na kusema ukweli andiko langu hili halitoweza hata kuandika robo ya yale yanayofahamika kitaalamu kuhusiana na pumu ya ngozi.
Maradhi haya kwa kifupi yamekuwa yakiathiri watoto wengi ulimwenguni na yamekuwa yakisumbua akili za wanasayansi na watabibu kote ulimwengu kwa muda mrefu.
Neno Eczema ambalo ndio jina la maradhi haya kwa kitaalamu ni neno la Kigiriki na linamaanisha kututumka sehemu ya nje ya ngozi, hali ambayo huonekana pale mtoto anapopata maradhi haya.
Maradhi haya ya ngozi yanachangia asilimia arobaini (40) ya maradhi yote ya ngozi yanayoripotiwa hospitalini.
Shambulizi lake
Maradhi haya hushambulia zaidi watoto na huweza kupitiliza mpaka ukubwani, pia lakini kwa wengi huwa yanapungua kadri mtoto anavyokua. Watafiti mbalimbali wanasema kuwa kumekuwa na ongezeko la maradhi haya katika kipindi cha miaka ya usoni hali inayoashiria kuwa maradhi haya ni ya kurithi (atopic eczema)
Karibu asilimia themanini (80) ya wagonjwa wa pumu ya ngozi huanza kuugua maradhi haya wakiwa chini ya umri wa miaka mitano (5). Wagonjwa wengi pia huonyesha dalili za maradhi haya wakiwa na umri chini ya mwaka mmoja.
Maradhi haya pia huweza kujitokeza ukubwani ingawa ni mara chache sana hali hii huonekana.
Maradhi haya huathiri watu wa jinsia zote kwa uwiano sawia yaani wanaume na wanawake.

Dalili zake
Maradhi haya ni ya muda mrefu nikimaanisha kuwa mtu huweza kukaa nayo kwa muda mrefu, ingawa si kuwa muda wote ngozi huonyesha dalili za maradhi. Watu wenye maradhi hupitia vipindi ambavyo ngozi hututumka na kuonyesha dalili za maradhi na vipindi ambavyo ngozi huonekana kama imepona ovyo kutoonyesha dalili yoyote ya maradhi.
Dalili za pumu ya ngozi ni kama zifuatazo:
-Sehemu ya ngozi iliyoathirika huwa inakuwa kavu (inaonekana kavu),
-Sehemu ya ngozi iliyoathirika huwa inatutumuka,
-Ngozi huwasha na kama ukikuna kwa muda mrefu basi hupasuka na kuweza kusababisha vidonda.
-Eneo la ngozi lililoathirika mara nyingine huuma.
-Ngozi huwa inakua na mipasuko inayoweza kuruhusu vimelea vya maradhi kushambulia sehemu za ndani za ngozi.
-Muwasho wa ngozi huwa mkali zaidi nyakati za usiku
-Maeneo yenye athari huwa yanavimba (au kututumka) na kuwa na joto.
-Maeneo ya ngozi yaliyoathirika huweza pia kuwa na malengelenge na hata kutoa majimaji.

Kama una swali,maoni au ushauri wasiliana nasi kwa simu 



namba 0769368546,0719097574 na 0754301115




pia 

www.facebook.com/lupimoclinic,www.twitter.com/lupimoclinic na www.hulkshare.com/lupimoclinic.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni