Jumatatu, 7 Desemba 2015

UFAHAMU UGONJWA WA PRESHA YA KUPANDA NA MATIBABU YAKE..[HYPERTENSION]

                                                                       

Hypertension ni nini? Huu ni ugonjwa ambao hugunduliwa pale presha ya damu inapokua juu sana kupita kiwango chake cha kawaida.

Kawaida damu inasukumwa na moyo kwenda sehemu mbalimbali za mwili lakini nguvu inayotumika kusukuma damu hiyo  kutoka moyoni kwenda sehemu zote za mwili na ile ambayo inakuwepo kwenye  mishipa ya damu wakati damu inapita ndio inaitwa presha ya damu. Hivyo binadamu yeyote lazima awe na presha ya damu lakini katika kiwango kinachohitajika ambacho ni 120\80mmhg mpaka 140\90mmhg zaidi ya hapo tunaita hypertension..

WALIOKWENYE HATARI YA KUPATA PRESHA..
umri mkubwa: wanaume wako katika hatari ya kupata presha kwenye umri wa miaka 45 na kuendelea na wanawake miaka 65 na kuendelea.

Rangi ya ngozi: presha ya damu inasumbua sana watu weusi na huweza kuanza katika umri mdogo zaidi na madhara makubwa kama kupooza, moyo kusimama ghafla na kufa kwa figo hutokea kwa weusi kuliko weupe.

Familia; Koo zenye wagonjwa wengi kwa presha kwani ugonjwa huu hufuata koo wakati mwingine

Unene: kadri unavyozidi kunenepa ndivyo mwili moyo unataka nguvu nyingi kusukuma damu 
mwilini hivyo kuongezeka kwa presha.

Kutofanya mazoezi

Kuvuta sigara: kemikali ya nikotini huharbu mishipa ya damu na kuongeza hatari ya kuugua ugonjwa wa presha.

Kula chumvi nyingi; sodium hubakiza maji mengi mwilini na kuongeza presha ya damu.

Kunywa pombe sana; kunywa zaidi ya bia mbili kwa wanaume na zaidi ya bia moja kwa wanawake ni hatari kwa moyo na hupandisha presha ya damu.

Mawazo mengi; mawazo mengi humwaga homoni inaitwa adrenaline kwenye damu ambayo huongeza presha ya damu hivyo maisha usiyachukulie serious sana matatizo ni sehemu ya maisha.

Magonjwa Fulani Fulani: magonjwa kama kisukari na magonjwa ya figo huongeza hatari ya kuugua presha ya damu.

Kuna aina mbili za presha ya kupanda..
Primary hypertension: ambayo inakumba zaidi ya 95% ya watu na chanzo chake hakifahamiki.

Secondary hypertension: ambayo inakuwepo kwa 5% ya watu na chanzo chake kinafahamika na ambavyo ni magonjwa ya figo, magonjwa ya mishipa ya damu, magonjwa ya ubongo na mishipa ya fahamu na magonjwa ya mfumo wa homoni.

dalili zake ni zipi?
Dalili za presha mara nyingi hua hazipatikani kirahisi na ugonjwa huu hauna dalili maalumu na wakati mwingine huja kulingana na chanzo cha presha hiyo kama nilivyoeleza kwenye secondary hypertension kama ifuatavyo.
  • Kichwa kuuma
  • Kutokwa damu puani.
  • Kupumua kwa shida.
  • Kuishiwa nguvu
  • Moyo kukimbia sana
  • Kutokwa jasho kwa wingi

Vipimo vinavyofanyika hospitali..
Kupima presha kwa kutumia kipimo cha presha kitaalamu kama sphygmomanometer ambacho ikiwa mgonjwa atapimwa mara tatu kwa siku tatu tofauti masaa na kukutwa presha yake iko juu ya kawaida atahesabiwa kama mgonjwa wa presha na matibabu yake yataanza haraka. hata hivyo mgonjwa anatakiwa apimwe baada ya dakika tano za kupumzika kama alikua kwenye mizunguko yake.

Vipimo vingine huchukuliwa na daktari kujaribu kujua chanzo cha ugonjwa na madhara ambayo mgonjwa anaweza kua ameshayapata kutokana na ugonjwa huo ni X ray ya moyo kuangalia ukubwa wa moyo, kuangalia wingi wa lehemu kwenye damu{cholesterol}, ultrasound za figo zote kuangalia kama kuna shida yeyote huku, kipimo cha maabara cha mkojo kuangalia kama figo zimenza kupitisha vitu visivyotakiwa kutoka kama damu na kadhalika na kupima sukari kuangalia kama mgonjwa ana kisukari kwani magonjwa haya huambatana mara nyingi.
 
kama unasumbuliwa na tatizo hilo la presha tufikie lupimo sanitarium clinic ambapo sisi hatutakupiga x-ray wala ultrasound bali tutakupima kwa kutumia vipimo vyetu vya mwili mzima ambavyo vitabaini tatizo hilo limekuathiri kwa kiasi gani  baada ya hapo tutakuanzishia dozi ambayo itarudisha presha yako kama ilivyokuwa awali, lupimo sanitarium clinic tunapatikana mikoa mbalimbali hapa nchini, unaweza kutufikia kati ya hii mikoa kwa matibabu zaidi.

VITUO VYETU TUNAVYOPATIKANA LUPIMO SANITARIUM CLINIC NI KAMA IFUATAYO. IRINGA TUPO KIHESA NJIA PANDA YA MTWIVILA, MBEYA TUPO SOWETO KARIBU NA UWANJA WA SHULE YA MSINGI MWENGE, DAR ES SALAAM TUPO SINZA MORI AU SINZA MAPAMBANO NYUMA YA UKUMBI WA LULU, DODOMA TUPO AREA C KARIBU NA MSIKITI WA AREA C, SINGIDA TUPO MANYONI NJIA PANDA YA KUELEKEA CHIKOLA NA HEKA, GEITA TUPO MITI MIREFU KARIBU NA BICK HOTEL, MWANZA TUPO NYEGEZI KITUO CHA KIJIWENI AU KALFONIA,


kwa maelezo zaidi,maoni au ushauri wasiliana nasi kwa simu namba 0769368546,0719097574 na 0742120577 pia www.facebook.com/lupimoclinic,www.twitter.com/lupimoclinic na www.hulkshare.com/lupimoclinic.
 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni