Jumatano, 6 Januari 2016

VIFAHAMU VIASHIRIA HIVI VINAVYOONESHA KUWA MWANAMKE YUPO TAYARI KUSHIKA UJAUZITO


Habari za leo mdau wa blog hii ya lupimo sanitarium clinic naamini utakuwa upo vizuri siku hii ya leo.

Naomba kuchukua muda wako mchache kwa ajili ya kufahamishana haya mambo muhimu ambayo huashiria mwanamke kuwa yupo tayari kwa asilimia nyingi kushika ujauzito.

Somo hili litawasaidia wale ambao wamekuwa wakitamani kuwa na watoto lakini hawafahamu ni siku gani sahihi ya kufanya tendo hilo la ndoa na wenzi wao ili kuweza kufanikisha kubeba ujauzito.

Sasa leo ninavyo viashiria ambavyo humaanisha mwanamke yupo katika hatari ya kuweza kushika ujauzito yaani 'ovulation period'

Kwanza kabisa mwanamke anapokuwa tayari kushika ujauzito huanza kuhisi hamu ya kushiriki tendo la ndoa, wanawake wanapokuwa katika siku zenye uwezekano mkubwa wa kushika mimba  matamanio yao ya kufanya mapenzi huwa ni makubwa zaidi kuliko ilivyo kawaida. Sasa huo ndio wakati unaofaa ikiwa unahitaji kubeba mimba au unahitaji mke wako abebe mimba.
Kupanda kwa joto la mwili, hii ni moja ya alama maarufu ambayo hutumiwa na wanawake wengi Ongezeko hilo la joto husababishwa na homoni ya 'progesterone', ambayo huongezeka sana
mara baada ya 'Ovulation'

Kubadilika kwa majimaji ya ukeni, wakati mwanamke anapokuwa katika uwezekano wa kushika mimba maji ya ukeni nayo huongezeka na kubadilika na kuwa katika hali ya majimaji na wakati mwingine huwa na rangi nyeupe kama yai bichi. Awali maji hayo ya ukeni huwa na rangi kama ya cream na hutoka kidogo sana na wengine hushindwa kuyaona kabisa.

Maumivu kwenye matiti, baadhi ya wanawake wakati wanapokaribia kwenye 'ovulation' huweza kuhisi maumivu kwenye matiti. Hata hivyo njia hii sio yenye kutegemewa sana kwani maumivu ya matiti huweza kusababishwa na masuala mengine kwani maumivu ya matiti hutokea kabla ya hedhi au baada ya kutumia baadhi ya dawa za kusaidia uzazi.
 
Ikumbukwe kwamba dalili zote hapo juu si lazima zitokee zote kila mwanamke huweza kuona dalili kati ya moja.Kuuelewa vyema mwili wako ni jambo zuri linaloweza kukusaidia kuzijua siku zako za 'Ovulation' na hivyo kuweza kujua siku zako za kubeba mimba.

Kwa elimu zaidi tufikie lupimo sanitarium clinic katika vituo vyetu vilivyopo mikoani,
 
VITUO VYETU TUNAVYOPATIKANA LUPIMO SANITARIUM CLINIC NI KAMA IFUATAYO. IRINGA TUPO KIHESA NJIA PANDA YA MTWIVILA, MBEYA TUPO SOWETO KARIBU NA UWANJA WA SHULE YA MSINGI MWENGE, DAR ES SALAAM TUPO SINZA MORI AU SINZA MAPAMBANO NYUMA YA UKUMBI WA LULU, DODOMA TUPO AREA C KARIBU NA MSIKITI WA AREA C, SINGIDA TUPO MANYONI NJIA PANDA YA KUELEKEA CHIKOLA NA HEKA, GEITA TUPO MITI MIREFU KARIBU NA BICK HOTEL, MWANZA TUPO NYEGEZI KITUO CHA KIJIWENI AU KALFONIA,


kwa maelezo zaidi,maoni au ushauri wasiliana nasi kwa simu namba 0769368546,0719097574 na 0742120577 pia www.facebook.com/lupimoclinic,www.twitter.com/lupimoclinic na www.hulkshare.com/lupimoclinic.


 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni