ZIFAHAMU FAIDA ZA LIMAO KAMA TIBA
Limao ni tunda dogo
ambalo mara nyingi hutumika jikoni katika shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja
na kukata shombo katika vyakula mbalimbali mfano samaki. Asili ya tunda hili ni
Asia.
zipo faida nyingi za kutumia limao, hasa wakati wa asubuhi
wakati mwili umekaa bila kula usiku kucha, miongoni mwa faida hizo ni pamoja na
kuusaidia mwili katika suala la mmeng’enyo wa chakula na kulifanya ini liweze
kufanya kazi vizuri.
Limao pia huwasaidia wale wenye matatizo ya tumbo, malaria, dosari katika figo, kiungulia na kuongeza hamu ya chakula.
Limao
husaidia wale wenye matatizo ya tumbo, kikohozi, mafindo findo, mafua,
kisukari, homa pamoja na kusaidia kuleta
harufu nzuri kinywani hii ni kwa sababu aside iliyopo kwenye maji ya limao
husaidia kuua bacteria walioko mdomoni wanaosababisha harufu mbaya ya kinywa,
ni vizuri ukatumia limao baada ya kusafisha meno.
malimao yana asid, ambayo ni chanzo kizuri cha vitamin C, ambayo ni nzuri kuzuia baridi na homa, lakini malimao pia husaidia kuzuia saratani ya damu.
Pumu, malengelenge, uvimbe na vidonda pia vyote hivyo huweza kutatulika
endapo mhusika atazingatia matumizi sahihi ya limao.
Pia maganda ya limao yanapotumika kwa kusugulia ngozi huwa ni dawa ya vipele, junjua na kuungua.
Pia maji ya limao
huweza kuondoa makovu na mikunjo kwenye ngozi na kupunguza makovu makubwa kama
ukinyunyizia kila mara. Hali kadhalika kutokana na uwezo wake wa kusafisha damu,
maji ya limao huacha ngozi ikiwa inang’aa na yenye afya.
kwa maelezo zaidi,maoni au ushauri wasiliana nasi kwa simu
namba 0769368546,0719097574 na 0742120577 pia
www.facebook.com/lupimoclinic,www.twitter.com/lupimoclinic na
www.hulkshare.com/lupimoclinictanzania,www.lupimoclinic.blogspot.com,youtube.com/lupimoclinic
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni