Jumapili, 10 Julai 2016




MKURUGENZI WA LUPIMO SANITARIUM CLINIC TABIBU JOHN LUPIMO AMEKABIDHI MADAWATI 50 YENYE THAMANI YA SHILLINGI MILLION 7 KATIKA HALMASHAURI YA KIDONDONI.



DC HAPI MADAWATI (3)

Serikali nchini imetakiwa kuhamishia nguvu waliyotumia katika upatikanaji wa madawati kwenye shule mbali mbali nchini  na kuelekeza katika ujenzi wa maabala na madarasa ili kuweza kumaliza tatizo hilo kwenye shule mbali mbali hapa nchini.DC HAPI MADAWATI (1)

Ombi hilo limetolewa na tabibu John Lupima ambaye ni  Tabibu Bingwa wa tiba mbadala kutoka kwenye kituo cha sayansi ya Tiba asili na tiba mbadala cha Lupimo  Sanitarium Clinic wakati alipokuwa anakabidhi madawati 50 yenye thamani ya milioni 7 katika Halmashauri ya Kinondoni, Ambapo amesema kwa licha ya serikali kuwekeza nguvu hadi kufanikiwa kukalibia kumaliza tatizo ukosefu wa madawati basi akaitaka serikali kuhamisha nguvu hiyo kwenye kumaliza tatizo la ukosefu wa madarasa pamoja na maabala ya kufundishia wanafunzi wa masomo ya sayansi jambo analodai litaweza kuikuza elimu nchini.DC HAPI MADAWATI (4)

Amesema kwa sasa kumekuwa na changoto kwenye baadhi ya shule kukosekana kwa madarasa ya kufundishia pamoja na Maabala ya kufundishia hadi kupelekea wanafunzi kufanya vibaya kwenye matokeo ya kidato cha nne, huku akibainisha kuwa  njia  sahihi ya kuweza kuinua elimu nchini na kuondoa changamoto ya wanafunzi kufanya vibaya kwenye matokea ni serikali kuongeza bidii katika kutatua tatizo hilo, Ameeleza kuwa hatua yake ya kusaidia madawati hayo yametokana na jitihada alizozionyesha Rais John Magufuli aliyoiweka katika kuhakikisha kuiboresha elimu hapa nchini.DC HAPI MADAWATI (5)

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Salum Hapi amemshukuru Tabibu huyo kwa mchango wake aliutoa wa madawati hayo huku akiwataka watu wengine wenye mapenzi ya kuisaidia elimu ya hapa nchini wajitokeze katika kusaidia mchango wa madawati ili tatizo liweze kutoweka kabisa ingawa kwa wilaya hiyo madawati sio tatizo kwani wilaya hiyo kwa kushirikiana na wadau walilimaliza mapema, hivyo madawati hayo ni kama ziada.

Tufikie sasa lupimo sanitarium clinic upate matibabu ya uhakika ambapo tunatibu kwa kutumia mimea mbogamboga na matunda.

 kwa maelezo zaidi,maoni au ushauri wasiliana nasi kwa simu namba 0769368546,0719097574 na 0742120577 pia www.facebook.com/lupimoclinic,www.twitter.com/lupimoclinic na www.hulkshare.com/lupimoclinictanzania,www.lupimoclinic.blogspot.com,youtube.com/lupimoclinic

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni