Jumamosi, 29 Oktoba 2016


UNAZIFAHAMU DALILI ZA SHAMBULIZI LA MOYO (HEART ATTACK)?



 
 Moja ya magonjwa hatari sana ambayo yanaweza kumpata mtu yoyote ni ugonjwa wa shambulizi la moyo. Huu ni miongoni mwa magonjwa yanayoongoza kwa kusababisha vifo vya wanaume na wanawake.

Kwa kawaida, ugonjwa huu hutokea pale ambapo sehemu ya nyama ya moyo inapoharibika au kufa kutokana na kukosa damu ya kutosha.


Je tatizo hili husababishwa na nini?
Husababishwa na kuziba kwa mishipa ya damu inayosambaza damu katika moyo (coronary artery blockage) kutokana na mafuta mabaya mwilini (atherosclerotic plaque).

Watu gani wapo katika hatari ya tatizo hili?
Watu walio katika hatari ya kukumbwa na ugonjwa huu ni pamoja na
• Wavutaji wa sigara
• Wenye umri mkubwa miaka 45 kwa wanaume na 55 kwa wanawake
• Watu wenye mafuta ya lijamu katika damu au wale wenye mafuta mabaya aina ya triglycerides na low density lipoprotein kwa kiwango kikubwa katika damu zao
• Wenye kisukari
• Wenye matatizo ya shinikizo la damu
• Walio na unene kupita kiasi (obesity)
• Wenye matatizo sugu ya kushindwa kufanya kazi kwa figo zao (chronic renal failure)
• Moyo kushindwa kufanya kazi (heart failure)
• Wanywaji wa pombe kupindukia
• Watumiaji wa madawa ya kulevya hasa cocaine na methamphetamine
• Watu wenye msongo wa mawazo (Chronic high stress levels)
• Upungufu wa vitamin B2, B6, B12 na folic acid

Dalili za shambulizi la moyo
• Maumivu makali ya ghafla kifuani ambayo husambaa kwenye taya, shingo, bega na mkono wa kushoto
• Kupumua kwa shida
• Kutoka jasho kwa wingi sana (diaphoresis)
• Kuhisi mapigo ya moyo yanapiga haraka (palpitations)
• Kichefuchefu
• Kutapika
• Kuchoka haraka sana
• Kupoteza fahamu
Shambulizi la moyo limehusishwa na nini?
Tafiti mbalimbali zimeusisha mambo yafuatayo na shambulizi la moyo
• Msongo wa mawazo
• Maambukizi hasa vichomi vinavyosababishwa na vimelea vya chlamydophila pneumonia.
• Hutokea zaidi asubuhi hasa saa tatu (saa 3 asubuhi)
 

Njia za kuzuia shambulizi la moyo
• Kuacha kuvuta sigara
• Kufanya mazoezi ya mara kwa mara
• Kupunguza unywaji wa pombe
• Kubadilisha aina ya mlo. Kupunguza mafuta katika mlo na chumvi.
• Kutumia mafuta ya samaki (omega-3 fatty acids)
• Kuna utafiti unaosema kuwa uchangiaji damu hupunguza hatari ya magonjwa ya moyo hasa kwa wanaume.
Madhara ya shambulizi la moyo
• Moyo kushindwa kufanya kazi (heart failure)
• Matatizo katika mfumo wa mapigo ya moyo (Atrial fibrillation) ambayo hatimaye hupelekea kifo
• Shambulizi la moyo kurudia mara ya pili
• Kifo cha ghafla (sudden death)


kwa maelezo zaidi unaweza ukanipigia kwa namba 0759324414

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni