Jumamosi, 2 Januari 2016


Ni wakati gani mazoezi hayaruhusiwi kwenye ujauzito?

Kwa mujibu wa maelekezo yaliyotolewa na Chuo Kikuu Cha Marekani cha Masuala ya Uzazi na Magonjwa ya Wanawake, mama mjamzito haruhusiwi kufanya mazoezi iwapo atakuwa na matataizo yafuatayo:
• Ugonjwa wa moyo.
• Ugonjwa wa mapafu.
• Kizazi kisichojitocheleza au kitaalamu cervical insufficiency/cerclage.
• Mimba ya mapacha, mapacha wawili, watatu na kuendelea na iwapo ana hatari ya kujifungua mapema kabla ya muda kutimia.
• Kutokwa na damu kunakoendelea katika miezi mitatu ya pili na ya tatu ya mimba.





• Mfuko wa uzazi ulioko upande wa chini wa kizazi au placenta previa. Hasa baada ya wiki 26 ya mimba.
• Uwezekano wa kujifungua mapema kabla muda haujatimia.
• Iwapo chupa imevunjika.
• Kifafa cha mimba (preeclamsia)
• Shinikizo sugu la damu.
• Ukosefu mkubwa wa damu.
• Kutokwa na majimaji ukeni.
• Ongezeko la mapigo ya moyo, hata wakati wa mapumziko.
Mama mjamzito pia anatakiwa kuzingatia dalili zifuatazo wakati anapofanya mazoezi, na anashauriwa kuacha haraka kufanya mazoezi anapohisi kuwa na dalili hizo:
• Kutoka damu ukeni.
• Kuhisi kizunguzungu au kuzimia, au kukosa nguvu.
• Kukosa pumzi au pumzi kumbana.
• Maumivu ya kichwa.
• Maumivu ya kifua.
• Misuli kukosa nguvu.
• Miguu kuuma na kuvimba.
• Maimivu ya mgongo na kiuno.
• Kujisikia uchungu au dalili za kujifungua kabla ya muda.
• Kupungua harakati ya mtoto ( kupungua hali ya kupiga mtoto tumboni)

kwa msaada zaidi unaweza pia kutufikia lupimo sanitarium clinic katika vituo vilivyopo mikoa mbalimbali hapa nchini.

VITUO VYETU TUNAVYOPATIKANA LUPIMO SANITARIUM CLINIC NI KAMA IFUATAYO. IRINGA TUPO KIHESA NJIA PANDA YA MTWIVILA, MBEYA TUPO SOWETO KARIBU NA UWANJA WA SHULE YA MSINGI MWENGE, DAR ES SALAAM TUPO SINZA MORI AU SINZA MAPAMBANO NYUMA YA UKUMBI WA LULU, DODOMA TUPO AREA C KARIBU NA MSIKITI WA AREA C, SINGIDA TUPO MANYONI NJIA PANDA YA KUELEKEA CHIKOLA NA HEKA, GEITA TUPO MITI MIREFU KARIBU NA BICK HOTEL, MWANZA TUPO NYEGEZI KITUO CHA KIJIWENI AU KALFONIA,


kwa maelezo zaidi,maoni au ushauri wasiliana nasi kwa simu namba 0769368546,0719097574 na 0742120577 pia www.facebook.com/lupimoclinic,www.twitter.com/lupimoclinic na www.hulkshare.com/lupimoclinic.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni