Msomaji wetu wa blog
hii ya lupimo sanitarium clinic karibu katika mwendelezo wa makala mbalimbali
zinazohusu afya yako zinazoletwa kwako na tabibu john lupimo wa lupimo
sanitarium ambapo leo anakuletea makala inayohusu ugonjwa wa saratani ya tezi dume
lakini
kama unaswali unaweza kuuliza kwa simu namba 0769368546,0719097574 na
0742120577 pia www.facebook.com/lupimoclinic,www.twitter.com/lupimoclinic na
www.hulkshare.com/lupimoclinic. au unaweza kutufikia katika vituo vyetu
vilivyopo mikoani VITUO VYETU TUNAVYOPATIKANA LUPIMO SANITARIUM CLINIC NI KAMA
IFUATAYO. IRINGA TUPO KIHESA NJIA PANDA YA MTWIVILA, MBEYA TUPO SOWETO KARIBU
NA UWANJA WA SHULE YA MSINGI MWENGE, DAR ES SALAAM TUPO SINZA MORI AU SINZA
MAPAMBANO NYUMA YA UKUMBI WA LULU, DODOMA TUPO AREA C KARIBU NA MSIKITI WA AREA
C, SINGIDA TUPO MANYONI NJIA PANDA YA KUELEKEA CHIKOLA NA HEKA, GEITA TUPO MITI
MIREFU KARIBU NA BICK HOTEL, MWANZA TUPO NYEGEZI KITUO CHA KIJIWENI AU
KALFONIA, Msomaji wetu mara baada ya kukumbusha mali na mawasiliano yetu
tunapopatikana sasa moja kwa moja twende kwenye makala yetu juu ya tatizo la
ugumba kwa mwanamke
Ugonjwa wa Saratani ya tezi dume
Tezi dume ni sehemu
mojawapo ya mfumo wa uzazi wa kiume. Inaundwa na sehemu mbili, lobes, ambazo
zimeunganishwa na kufunikwa kwa nje kwa utando wa tishu.
Tezi hii ipo mbele
kidogo ya puru (rectum) na na chini kidogo ya kibofu cha mkojo. Tezi dume
inauzunguka mrija unaounganisha kibofu cha mkojo na uume (urethra)
Watu wengi wamekuwa na shauku ya kutaka kujua ugonjwa wa saratani ya tezi dume, huku wakidhani ni mpya. Lakini ukweli ni kuwa umekuwapo miaka mingi na wengi wameugua.
Watu wengi wamekuwa na shauku ya kutaka kujua ugonjwa wa saratani ya tezi dume, huku wakidhani ni mpya. Lakini ukweli ni kuwa umekuwapo miaka mingi na wengi wameugua.
Takwimu
zinaonyesha wanaume wengi huugua ugonjwa huu unaoongezeka kwa kasi ya hali ya
juu.
Kulingana
na utafiti uliofanywa na Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORIC), kutoka mwaka
2006, zinaonyesha kuwa kila mwaka kumekuwa na ongezeko la kesi mpya ya wagonjwa
saratani ya tezi dume.
Novemba
ya kila mwaka, jumuiya za kimataifa huadhimisha tukio ambalo hujulikana kama
Movemba.
Maadhimisho
hayo huhusisha kukuza kwa masharubu, kukusanya fedha na kuleta mwamko na
ufahamu wa masuala ya afya kwa wanaume kama vile saratani ya tezi dume.
Jina
hilo la Movemba ni mchanganyiko wa neno ‘Masharubu na Novemba’.
Maadhimisho
hayo ya mwezi mzima yanalenga kuongeza ufahamu na mwamko kwa kupima ili
kugundua mapema.
Mwaka
jana peke yake zaidi ya Dola za Marekani 120 milioni zilikusanywa.
Hadi
sasa, Movemba imekusanya zaidi ya Dola 550 milioni kupitia wanachama wake
milioni nne katika nchi 21 duniani kote.
Waziri
mstaafu wa Afya na Ustawi wa Jamii, Profesa David Mwakyusa alinukuliwa akisema
asilimia 10 ya wagonjwa wanaosumbuliwa na aina mbalimbali za saratani
wamejitokeza hospitalini kwa uchunguzi na matibabu.
Anasema
asilimia 90 iliyobaki hawajafanya jitihada zozote kuhudhuria uchunguzi na
matibabu.
Akizungumzia
juu ya uchunguzi wa hali ya tezi dume nchini, Mwanzilishi na Mwenyekiti wa
Hospitali ya Apollo yenye makao makuu India, Dk Prathap Reddy anasema kuwa
ugonjwa huo unaathiri watu wengi na kusababisha vifo vingi nchini kwa sababu ya
ukosefu wa ufahamu wa kina juu ya ugonjwa huo.
Utaratibu
wa uchunguzi wa saratani ya tezi dume haufanyiki kutokana na gharama na ukosefu
vifaa vya uchunguzi nchini.
Watu
wengi hurejea hospitali wakati ugonjwa huo upo katika hatua ya mwisho na
hauwezi kuzuilika tena. Hata hivyo, kuna uwezekano wa ugonjwa huo kutibika
endapo utagundulika mapema.
Pamoja
na kuwapo kifaa maalumu cha utambuzi wa saratani ya tezi dume ‘chaprostate
specific antigen’ (PSA) duniani, Watanzania wachache wana uwezo wa kupata
huduma hii.
Kwa
sababu kifaa hiki kina gharama kubwa na kinahitaji wafanyakazi wenye ujuzi na
upimaji wenyewe ni gharama kubwa.
Mchungaji
Dk Emmanuel Kandusi aliyenusurika na saratani ya tezi dume ana uzoefu wa
kutosha juu ya ugonjwa huu na anajaribu kujenga ufahamu na uelewa kwa wananchi
wenzake.
Tofauti
na Watanzania wengi Dk Kandusi alikuwa na uwezo wa kupata matibabu ushauri
kutoka nje ya nchi.
Wakati
akiugua alikuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Apollo.
“Kutokana
na maendeleo na upatikanaji wa vifaa muhimu na wafanyakazi wa kutosha katika
hospital hiyo nilikuwa na uwezo wa kuokoa maisha yangu na kuanza kuwaelimisha
wengine,” anasema.
Saratani
ya tezi dume ni aina ya saratani ambayo huanzia kwenye tezi za kibofu ya jinsia
ya kiume itokanayo na ukuaji hafifu wa seli inayopelekea uvimbe katika tezi.
Baada
ya hapo seli za saratani husambaa kutoka kwenye tezi dume kwenda sehemu
nyingine za mwili hususan katika mifupa na matezi ambayo husababisha maumivu
hasa katika kupitisha haja ndogo na wakati wa tendo la ndoa.
Hii
ni aina ya saratani ambayo hushambulia zaidi wanaume walio juu ya miaka 50.
Tafiti
zilizofanyika hivi karibuni zinaonyesha kuwa wanaume walio chini ya miaka 40
wana uwezo wa kupata saratani ya tezi dume kwa uwiano wa mtu mmoja kati ya
100,000.
Kwa
wanaume walio kati ya miaka 70 na 74 wako katika hatari ya kupata saratani hiyo
kwa wastani wa watu 1,326 kati ya 100,000.
Hali
kadhalika inakisiwa mwanamume mmoja kati ya sita hupata saratani ya tezi dume
katika maisha yao .
Kila
mwaka kati ya wanaume wote wanaogundulika na saratani moja ya nne wana saratani
ya tezi dume.
Desmond
Tutu anasema ugonjwa huu wa saratani ya tezi dume kuwa hauna mipaka ya kijamii.
Dalili
Dalili
za tezi dume ni matatizo katika mfumo wa haja ndogo pamoja na kwenda haja mara
kwa mara hususan usiku na kushindwa kuistahimili kwa muda.
Nyingine
ni matone ya damu kati haja ndogo, maumivu katika sehemu ya chini ya mgongo,
upotevu wa hamu ya kula na kupungua uzito.
Ili
kugundua saratani ya tezi dume, mgonjwa anahitaji uchunguzi wa kina katika njia
yake ya haja ndogo ambako daktari hujaribu kuhisi uvimbe wowote utakao kuwa
katika mfumo wa mkojo na matezi uchunguzi ambao hufuatiwa na vipimo vya damu.tatizo hili lupimo sanitarium clinic tunalitibu vizuri sana chakufanya tufikie haraka sana katika vituo vyetu vilivyopo mikoani
VITUO VYETU
TUNAVYOPATIKANA LUPIMO SANITARIUM CLINIC NI KAMA IFUATAYO. IRINGA TUPO KIHESA
NJIA PANDA YA MTWIVILA, MBEYA TUPO SOWETO KARIBU NA UWANJA WA SHULE YA MSINGI
MWENGE, DAR ES SALAAM TUPO SINZA MORI AU SINZA MAPAMBANO NYUMA YA UKUMBI WA
LULU, DODOMA TUPO AREA C KARIBU NA MSIKITI WA AREA C, SINGIDA TUPO MANYONI NJIA
PANDA YA KUELEKEA CHIKOLA NA HEKA, GEITA TUPO MITI MIREFU KARIBU NA BICK HOTEL,
MWANZA TUPO NYEGEZI KITUO CHA KIJIWENI AU KALFONIA,
kwa maelezo
zaidi,maoni au ushauri wasiliana nasi kwa simu namba 0769368546,0719097574 na
0742120577 pia www.facebook.com/lupimoclinic,www.twitter.com/lupimoclinic na
www.hulkshare.com/lupimoclinic.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni