Wednesday, February 3, 2016
Sakata La Mauaji Ya Diwani Wa CUF Lachukua Sura Mpya
habari inaletwa kwako kwa udhamini mkubwa wa lupimo sanitarium clinic kwa matibabu mazuri ya kiafya, na maradhi sugu, kama muwasho sehemu za siri, kutokupata ujauzito nguvu za kiume vidonda vya tumbo, na mengine mengi, mawasiliano yetu ni 0769368546 au 0719097574 karibu sana
Mauaji
ya kikatili ya Diwani wa Kata ya Kimwani, Wilaya ya Muleba mkoani
Kagera, Sylvester Muliga (CUF), yameanza kuibua mambo mazito huku
ikielezwa kuwa Ijumaa alikuwa awasilishe hoja kwenye Baraza la Madiwani
kuhusu masuala ya ardhi.
Muliga
ambaye alifia Hospitali ya Kagondo alikopelekwa kwa matibabu baada ya
kukatwa mapanga Jumapili usiku, imeelezwa kuwa katika kikao hicho
ilikuwa aombe kuundwa kwa kamati ya kuchunguza uhalali wa maeneo makubwa
ya ardhi yanayomilikiwa na watu wachache.
Kwa
mujibu wa mjumbe wa Kamati ya Uchumi na Mazingira ambaye pia ni Diwani
wa Kata ya Kasharunga, Khalid Swalehe, hoja hiyo ilikuwa iwasilishwe na
Muliga na ilikuwa inaungwa mkono na madiwani wa kata zote zilizo na
migogoro ya ardhi.
Baada
ya taarifa za kufariki dunia kwa diwani huyo, wananchi walivamia nyumba
nane za watuhumiwa wanaodaiwa kutekeleza mauaji hayo na kuziteketeza
kwa moto.
Pia, walichoma moto mashine mbili za kusaga na kuharibu gari la mmoja wa wagombea wa udiwani katika Uchaguzi Mkuu uliopita.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kijiji cha Kyota, Daudi Kiruma, wananchi wamehusisha mauaji hayo na mambo ya siasa.
“Kinachoonekana hapa baadhi ya watu wanataka kupotosha ajenda ili wahusika wa mauaji wapate nafasi ya kutoroka,” alisema Kiruma.
Hata hivyo, Kiruma alisema hana uhakika kama mtuhumiwa anayedaiwa alikuwa mgombea amekamatwa, kwa sababu haonekani.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Kagera, Augustine Ollomi, jana alisema wanamshikilia
mtuhumiwa mwingine ambaye anafanya idadi ya walikomatwa kuhusiana na
mauaji hayo kufikia watatu mpaka sasa.
Kamanda Ollomi aliwataka wananchi wasijadili mauaji hayo kwa hisia za kisiasa bali waviachie vyombo vya dola vifanye kazi yake.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
VITUO VYETU
TUNAVYOPATIKANA LUPIMO SANITARIUM CLINIC NI KAMA IFUATAYO. IRINGA TUPO KIHESA
NJIA PANDA YA MTWIVILA, MBEYA TUPO SOWETO KARIBU NA UWANJA WA SHULE YA MSINGI
MWENGE, DAR ES SALAAM TUPO SINZA MORI AU SINZA MAPAMBANO NYUMA YA UKUMBI WA
LULU, DODOMA TUPO AREA C KARIBU NA MSIKITI WA AREA C, SINGIDA TUPO MANYONI NJIA
PANDA YA KUELEKEA CHIKOLA NA HEKA, GEITA TUPO MITI MIREFU KARIBU NA BICK HOTEL,
MWANZA TUPO NYEGEZI KITUO CHA KIJIWENI AU KALFONIA,
kwa maelezo
zaidi,maoni au ushauri wasiliana nasi kwa simu namba 0769368546,0719097574 na
0742120577 pia www.facebook.com/lupimoclinic,www.twitter.com/lupimoclinic na
www.hulkshare.com/lupimoclinic.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni