Jumatatu, 25 Januari 2016

     FAHAMU KUHUSU SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI


Kwanza kabisa shingo ya kizazi, hii  ni njia ya kizazi kati ya uke na mji wa mimba. Sehemu hiyo ina kazi nyingi ikiwa ni pamoja na kupitisha mbegu za kiume kuelekea katika mirija ya uzazi ili kupevusha yai,.

Kazi nyingine ya shingo ya kizazi ni kupitisha damu ya hedhi na pia ndio mlango anaopitia mtoto wakati wa kuzaliwa. 

Saratani ya shingo ya kizazi ni mabadiliko ya chembe chembe hai zilizo juu au zinazofanana na shingo ya uzazi, lakini kwa mujibu wa watalaam huainisha kuwa saratani hiyo ya shingo ya kizazi husababishwa na kuanza ngono mapema katika umri mdogo chini ya miaka 18.

Pia saratani hiyo huweza kutokea kwa  kuwa na wapenzi wengi na kuvuta sigara. Pia miongoni mwa mambo yanayochangia kupata saratani ya shingo ya kizazi ni pamoja na historia ya kubeba mimba nyingi na unywaji pombe kupindukia huku watu walioathirika na virusi vya Ukimwi wakiwa katika hatari zaidi ya kupata maradhi hayo.

Hata hivyo, kimsingi ugonjwa huu husababishwa na virusi vinavyoitwa Human papilloma, ambapo mtu anaweza kupatwa na virusi hawa wakati wa kujamiana na mtu mwenye maambukizi. 

Miongoni mwa dalili ambazo huashirira tatizo hili ni pamoja na kutokwa na damu ambayo si ya hedhi, kutokwa na uchafu, majimaji au usaha sehemu za siri.

Dalili nyingine ni kuhisi maumivu makali wakati wa kujamiiana na kusababisha kutokwa na damu baada ya tendo hilo, pia maumivu hayo huweza kuambatana na maumivu ya tumbo chini ya kitovu sambamba na maumivu ya kiuno.

Ili kuepuka tatizo hili ni vyema kujenga utaratibu wa kwenda kuchunguza afya mara kwa mara angalau mara moja kila mwaka siku zote wahenga husema kinga ni bora kuliko tiba, basi tufahamu kuwa kwa kujikinga tunaweza kujiepusha na magonjwa mengi na hata haya ya saratani. 

Njia nzuri ya kuepukana na magonjwa haya ni pamoja na kujichunga kitabia na kutofanya ngono zembe.
 
mawasiliano yetu ya lupimo sanitarium clinic kwa matibabu ya ugonjwa huo wa saratani ya shingo ya kizazi, tufikie katika mikoa tunayopatikana

VITUO VYETU TUNAVYOPATIKANA LUPIMO SANITARIUM CLINIC NI KAMA IFUATAYO. IRINGA TUPO KIHESA NJIA PANDA YA MTWIVILA, MBEYA TUPO SOWETO KARIBU NA UWANJA WA SHULE YA MSINGI MWENGE, DAR ES SALAAM TUPO SINZA MORI AU SINZA MAPAMBANO NYUMA YA UKUMBI WA LULU, DODOMA TUPO AREA C KARIBU NA MSIKITI WA AREA C, SINGIDA TUPO MANYONI NJIA PANDA YA KUELEKEA CHIKOLA NA HEKA, GEITA TUPO MITI MIREFU KARIBU NA BICK HOTEL, MWANZA TUPO NYEGEZI KITUO CHA KIJIWENI AU KALFONIA,


kwa maelezo zaidi,maoni au ushauri wasiliana nasi kwa simu namba 0769368546,0719097574 na 0742120577 pia www.facebook.com/lupimoclinic,www.twitter.com/lupimoclinic na www.hulkshare.com/lupimoclinic.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni