FAHAMU KUHUSU SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI
Kwanza kabisa shingo ya kizazi, hii ni njia ya kizazi kati ya uke na mji wa mimba. Sehemu hiyo ina kazi nyingi ikiwa ni pamoja na kupitisha mbegu za kiume kuelekea katika mirija ya uzazi ili kupevusha yai,.
Kazi nyingine ya shingo ya kizazi ni kupitisha damu ya hedhi na pia ndio mlango anaopitia mtoto wakati wa kuzaliwa.
Saratani ya shingo ya kizazi ni mabadiliko ya chembe chembe hai
zilizo juu au zinazofanana na shingo ya uzazi, lakini kwa mujibu wa
watalaam huainisha kuwa saratani hiyo ya shingo ya kizazi husababishwa
na kuanza ngono mapema katika umri mdogo chini ya miaka 18.
Pia saratani hiyo huweza kutokea kwa kuwa na wapenzi wengi na kuvuta
sigara. Pia miongoni mwa mambo yanayochangia kupata saratani ya shingo
ya kizazi ni pamoja na historia ya kubeba mimba nyingi na unywaji pombe
kupindukia huku watu walioathirika na virusi vya Ukimwi wakiwa katika
hatari zaidi ya kupata maradhi hayo.
Hata hivyo, kimsingi ugonjwa huu husababishwa na virusi vinavyoitwa Human papilloma, ambapo mtu anaweza kupatwa na virusi hawa wakati wa kujamiana na mtu mwenye maambukizi.
Hata hivyo, kimsingi ugonjwa huu husababishwa na virusi vinavyoitwa Human papilloma, ambapo mtu anaweza kupatwa na virusi hawa wakati wa kujamiana na mtu mwenye maambukizi.
Miongoni mwa dalili ambazo huashirira tatizo hili ni pamoja na
kutokwa na damu ambayo si ya hedhi, kutokwa na uchafu, majimaji au usaha
sehemu za siri.
Dalili nyingine ni kuhisi maumivu makali wakati wa kujamiiana na
kusababisha kutokwa na damu baada ya tendo hilo, pia maumivu hayo huweza
kuambatana na maumivu ya tumbo chini ya kitovu sambamba na maumivu ya
kiuno.
Ili kuepuka tatizo hili ni vyema kujenga utaratibu wa kwenda kuchunguza afya mara kwa mara angalau mara moja kila mwaka siku zote wahenga husema kinga ni bora kuliko tiba, basi tufahamu kuwa kwa kujikinga tunaweza kujiepusha na magonjwa mengi na hata haya ya saratani.
Njia nzuri ya kuepukana na magonjwa haya ni pamoja na kujichunga kitabia na kutofanya ngono zembe.
mawasiliano yetu ya lupimo sanitarium clinic kwa matibabu ya ugonjwa huo wa saratani ya shingo ya kizazi, tufikie katika mikoa tunayopatikana
VITUO VYETU
TUNAVYOPATIKANA LUPIMO SANITARIUM CLINIC NI KAMA IFUATAYO. IRINGA TUPO KIHESA
NJIA PANDA YA MTWIVILA, MBEYA TUPO SOWETO KARIBU NA UWANJA WA SHULE YA MSINGI
MWENGE, DAR ES SALAAM TUPO SINZA MORI AU SINZA MAPAMBANO NYUMA YA UKUMBI WA
LULU, DODOMA TUPO AREA C KARIBU NA MSIKITI WA AREA C, SINGIDA TUPO MANYONI NJIA
PANDA YA KUELEKEA CHIKOLA NA HEKA, GEITA TUPO MITI MIREFU KARIBU NA BICK HOTEL,
MWANZA TUPO NYEGEZI KITUO CHA KIJIWENI AU KALFONIA,
kwa maelezo
zaidi,maoni au ushauri wasiliana nasi kwa simu namba 0769368546,0719097574 na
0742120577 pia www.facebook.com/lupimoclinic,www.twitter.com/lupimoclinic na
www.hulkshare.com/lupimoclinic.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni