JIFUNZE NAMNA YA KUKABILIANA NA UGONJWA WA PUMU
Pumu ni miongoni mwa magonjwa sugu ya hewa
yanayosumbua idadi kubwa ya watu duniani na hasa watoto, huku idadi ya
wanaokabiliwa na tatizo hili ikionekana kuongezeka siku hadi siku.
Mtaalam wa tiba mbadala tabibu john lupimo anaanza kwa kusema kuwa “kwa kawaida
binadamu anapovuta pumzi/ hewa huenda kwenye mdomo au pua kupitia katika mirija
ya hewa na kusafiri hadi kwenye mapafu katika mlolongo huu wa usafirishaji hewa
kupitia mirija yake , tatizo la pumu huibuka pindi njia hizo zinapoingiliwa na
kitu kutoka nje na kusababisha ugumu katika upumuaji”
Aidha, mtaalam huyo anasema kwa kiasi kikubwa tatizo
hili la pumu hupatikana kwa njia ya kurithi na hasa kwa wale watu wenye
matatizo ya mzio (allergy)
Ugonjwa wa pumu umegawanyika katika makundi mawili,
ambapo aina ya kwanza ya ugonjwa huu hutokana na matatizo ya kurithi hasa kwa
wale watu wenye matatizo ya mzio (allergy)
hivyo aina hii hufahamika kwa jina la ‘allergic
asthma’ ambayo ipo sana kwenye nchi za kiafrika ikiwemo Tanzania.
Aina hii ya kwanza ya pumu kwa sehemu kubwa
husababishwa na chavua (pollen),
ukungu (fog), wanyama pamoja na
chembechembe za vumbi n.k, lakini pia aina hii ya pumu huweza kuingia mwilini
kupitia kitu chochote kilicholiwa mfano samaki. nk.
Manyoya ya wanyama wa kufungwa pia ni hatari kwa mtu
mwenye pumu kwani husababisha kuchochea shambulizi la pumu ya mzio (allergy) au ‘allergic ‘asthma’
Aina ya pili ya ugonjwa huu wa pumu hufahamika kwa
jina la ‘non allergic asthma’ hii
haitokani na matatizo ya mizio au kurithi kutoka kizazi kilichopita, hivyo
huweza kumpata mtu yeyote kwani aina hii husababishwa na hewa kavu, baridi
kali, mazoezi, moshi, manukato yenye harufu kali, msongo wa mawazo, nk.
Dalili za ugonjwa huu hazitofautiani kutokana na
vyanzo vyake bali zote hufanana na hujitokeza sawa katika mwili wa mwanadamu na
miongoni mwa dalili hizio ni pamoja na kifua kubana, kikohozi kikavu, mapigo ya
moyo kwenda mbio, kukosa hewa ya kutosha kwenye mirija, kuhisi baridi.
Mtu mwenye tatizo la pumu hushauriwa mara
anapojigundua kuwa anashida hii anapaswa kumuona daktari ili kufanyiwa vipimo
zaidi vya kina na kugundua chanzo cha tatizo lake na jinsi ya kukabiliana nalo.
Hata hivyo, tabibu john lupimo anasema unaweza kuepukana na
maradhi haya kwa kuepuka kukaa maeneo yanayochangia shambulizi la pumu kwako
kutokana na maelezo ya daktari wako, epuka pia vipodozi vya manukano yenye
harufu kali ambayo pia kula vyakula
vyenye asili ya mboga za majani kama vile nyanya, bilinganya, maharage, matango
na vyote vyenye asili hiyo.
Kama
unngependa kuonana na kuzungumza vizuri na mtaalamu tabibu john lupimo kuhusu
tatizo la la kiafya fika sasa lupimo sanitarium clinic tunapatikana mikoa mbali mbali hapa nchini
VITUO VYETU
TUNAVYOPATIKANA LUPIMO SANITARIUM CLINIC NI KAMA IFUATAYO. IRINGA TUPO KIHESA
NJIA PANDA YA MTWIVILA, MBEYA TUPO SOWETO KARIBU NA UWANJA WA SHULE YA MSINGI
MWENGE, DAR ES SALAAM TUPO SINZA MORI AU SINZA MAPAMBANO NYUMA YA UKUMBI WA
LULU, DODOMA TUPO AREA C KARIBU NA MSIKITI WA AREA C, SINGIDA TUPO MANYONI NJIA
PANDA YA KUELEKEA CHIKOLA NA HEKA, GEITA TUPO MITI MIREFU KARIBU NA BICK HOTEL,
MWANZA TUPO NYEGEZI KITUO CHA KIJIWENI AU KALFONIA,
kwa maelezo
zaidi,maoni au ushauri wasiliana nasi kwa simu namba 0769368546,0719097574 na
0742120577 pia www.facebook.com/lupimoclinic,www.twitter.com/lupimoclinic na
www.hulkshare.com/lupimoclinic.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni