Ijumaa, 15 Januari 2016

Tatizo la Uvimbe kwenye mfuko wa uzazi(Uterine fibroid)

Uvimbe kwenye mfuko wa uzazi hutokea kwenye misuli laini (smooth muscle) ya mfuko wa uzazi. Ni uvimbe ambao siyo saratani(benign tumor). Majina yalizoeleka ni myoma au uterine fibroid.

Myoma ni aina ya uvimbe ambao  unaowaathiri  wanawake wengi hasa katika umri wa  miaka
   ya uzazi.

Dalili
Uvimbe  ukiwa mdogo unaweza usiwe na dalili zozote. Dalili hutegemea sehemu ulipo kwenye mfuko wa uzazi na ukubwa wake. Hatahivyo dalili zake ni kuvuja damu bila kufuata mpangilio wa mzunguko wa mwanamke, kutoka damu nyingi au maumivu wakati wa hedhi, maumivu ya tumbo, maumivu ya mgogo, kukojoa mara kwa mara au mkojo kujifungia na wakati mwingine  ugumba.

Pia mwanamke anaweza kusikia maumivu wakati wa kujamiiana, na huweza kusababisha mimba kutoka.
Ingawaje wanawake wengi hupata uvimbe kwenye mfuko wa uzazi lakini sio sababu hasa ya ugumba au utasa.

Uchunguzi
Daktari anaweza kuhisi uvimbe kwa kutumia mikono miwili anapokuwa ana pima tumbo;hatahivyo kipimo cha Ultrasound ya nyonga hutumika kugundua uvimbe kwenye kizazi cha mwanamke. MRI pia huweza kutumika kupata usahihi wa ukubwa na eneo uvimbe ulipo.

Tatizo hili mara nyingi huambatana na maradhi mengine.Maradhi hayo ni kama
.Upungufu wa damu
.Kufunga choo
.matatizo ya fingo
.mara  chache huweza  saratani

Matibabu
Matibabu ya tatizo hili yanaweza kulenga kutibu dalili, au kupunguza uvimbe. Hata hivyo kama ugonjwa huu hauna dalili unaweza kutazamiwa tu bila kuchukua hatua zozote. Mwanamke akikoma siku zake tatizo hili huwa linatoweka. 

NB: Kwa upande wa lupimo sanitarium clinic tuafanya nini kwa ajili ya kukutibu tatizo lako hilo la uvimbe sisi tutakupima kwanza tuangalie uvimbe huo umekuwa kiasi gani baada ya hapo tutakupatia dawa ya kuyeyusha huo uvimbe ukaisha kabisa na ieleweke ya kwamba lupimo sanitarium clinic hatufanyi upasuaji bali tunakupa dawa ya kuyeyusha huo uvimbe 
kwa msaada zaidi na mawasiliano unaweza kutufikia lupimo sanitarium clinic katika vituo vyetu vilivyopo mikoa mbalimbali hapa nchini, 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni