Lupimo sanitarium clinic ni
kituo cha tiba asili wanatibu magonjwa kama
kuota kinyama sehemu ya haja kubwa na magonjwa mengine mengi, kutana tabibu
bingwa ambae ni mkurugenzi wa lupimo sanitarium clinic John lupimo mpigie simu
sasa hivi umweleze tatizo lako kupitia 0742120577,0769368546 au 0672666601.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Naibu Kamishna Simon Sirro.
Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam limefanikiwa kukamata
magari mawili yakihusishwa na wizi katika ofisi ya kamshina mkuu wa TRA
huku yakiwa na vifaa vilivyoibiwa katika ofisi hiyo vikiwa ni pamoja na
komputa, na TV.
Katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam
kamanda Simon Sirro amesema kutokana na oparasheni kali iliyokuwa
ikiendeshwa na jeshi ilifanikiwa kuwatia nguvuni watuhumiwa wanne wakiwa
na vifaa vilivyoibiwa.
Aidha kamanda huyo wa kanda maalum ya Dar es Salaam amesema katika
oparesheni hiyo pia jeshi la polisi lilifanikiwa kuokoa zaidi ya
shilingi milioni 150 mali ya Bw Ahmed Huwel mkazi wa Msasani.
Katika hatua nyingine Kamanda Sirro ametangaza kusitishwa kwa muda
kwa shughuli za ulinzi shirikishi katika vituo vya polisi kutokana na
vikundi hivyo kualamikiwa na wananchi kwa kutokuwa na tija katika jamii
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni